Wednesday, August 10, 2011
Biblia inasema nini juu ya kamari? Je, kamari ni dhambi?
Swali: "Biblia inasema nini juu ya kamari? Je, kamari ni dhambi?"
Jibu: Kamari ni “pesa zinazohatarishwa katika jaribio la kuzizidisha kwa njia isiyo ya kawaida.” Bibilia haipingi moja kwa moja kamari,bahati nasibu na kadhalika. Biblia hutuonya tujiepushe na tamaa ya pesa. (Timotheo wa kwanza 6:10; waebrania 13;5). Maandiko pia husisitiza tuepukane na nia ya kutaka kujitajirisha haraka haraka (Methali 13:11; 23:5; Mhubiri 5:10). Kamari imekithiri katika msingi wa tamaa ya pesa na hutia watu katika majaribu ya kutaka kuwa tajiri upesi.
Kamari ina ubaya gani? Inapofanywa mara kwa mara ina asili ya matumizi mabaya ya pesa si lazima yenyewe iwe ni dhambi. Ijapokuwa kuna mambo mengi ambayo yanaweza kuleta matumizi mabaya ya pesa kama kununua chakula cha ghali bila sababu ya maana au kununua vitu visivyofaa lakini isiwe sababu ya kuhalalisha kamari. Pesa zisifujwe. Pesa ni zihifadhiwe kwa matumizi mazuri ya baadaye lakini sio kamari.
Kamari katika Biblia: ijapokuwa biblia haitaji moja kwa moja michezo ya kamari, huzungumzia michezo Fulani ya bahati nasibu kama kupiga kura katika Mambo ya Walawi kuchagua baina ya mbuzi wa sadaka na mbuzi wa lawama. Yoshua alipigia kura ugawaji wa ardhi kwa makabila mbali mbali. Nehemia alipiga kura kutambua nani atakayeishi ndani ya nyua za Yerusalemu na nani asiishi ndani yake. Mitume walipiga kura kuchagua atakaye chukua nafasi ya Yuda. Methali 16:33 inasema, “ kura hupigwa mapajani lakini uamuzi hutoka kwa Bwana.” Hakun mahali katika Biblia kubahatisha kumetumika kwa starehe ama kuendelezwa kama jambo halali la wafuasi wa Mungu.
Kasino na bahati nasibu: Kasino hutumia mbinu nyingi kuhamasisha wacheza kamari kuendelea kupoteza pesa nyingi zaidi. wakati mwingine hutoa vileo kwa bei nafuu au hata bure kinachorahisisha kulewa ili mtu asiweze kufanya uamuzi tena wa busara kwa kuwa amelewa sana. Kila kitu ndani ya kasino kimeundwa kuchukua pesa za watu kwa wingi bila kurudishia chochote mwenye kutoa pesa hizo. Michezo ya bahati nasibu husingiziwa kuwa ni ya kusaidia kuchangia elimu au huduma za kijamii. Lakini wenye kucheza michezo hii ni wale wenye pesa za kununulia kadi hizi za bahati nasibu. Tamaa ya kutajirika haraka huwashika wenye kushiriki hivyo basi wanapokosa kufanikiwa huwabakisha katika hali mbaya zaidi ya ile ya awali. Hapa ndipo maisha ya wengi husambaratika.
Kwa nini mapokeo kutoka kwa bahati nasibu hayamridhishi Mungu: wengi husema wanacheza michezo hiyo ili watoe pesa hizo kwa kanisa au kufanyia jambo Fulani zuri. Hili ni jambo zuri. Lakini uchunguzi umedhihirisha mara nyingi si kwa ajili ya mambo haya. Mungu hahitaji pesa zetu kuendeleza kazi zake duniani. Methali 13:11 inasema, “ pesa mbaya hutoroka zenyewe, lakini yule akusanyaye pesa chache chache huzifanya kukua na kuwa nyingi.” Mungu ni muweza na atagharimia mahitaji ya kanisa kwa njia za halali. Je, Mungu angeheshimiwa kwa kupokea mchango wa pesa zilitokana na biashara ya madawa ya kulevya au zilizoibwa benki? Hata hivyo Mungu hahitaji pesa zilizoibwa kwa maskini katika jaribio la kutaka kuwa matajiri haraka.
Timotheo wa kwanza 6:10 inatuambia, “maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na imani, na kujichoma kwa maumivu mengi.” Waebrania 13:5 inasema, “ msiwe na tabia ya kupenda fedha mwe radhi na vitu mlivyo navyo;kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa.” Mathayo 6:24 inasema, “ hakuna awezaye kuwatumikia mabwana wawili. Kwa maana atamchukia huyu na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu na kumdharau huyu.hmwezi kumtumikia Mungu na mali.”
Tuesday, June 7, 2011
Tuesday, May 31, 2011
SOMO:SIKU ZA MWISHO
Makafiri hawaamini yakuwa dunia inakaribia kisha na mwisho ukaribu. Imeandikwa 2Petero 3:3-4 "Mkijua kwanza neno hili ya kwamba katika siku za mwisho kutakuja na dhihaka za watu wenye kudhihaki wafuatao tamaa za wenyewe na kusema ikowapi ahadi ile ya kuja kwake kwa maana tangu hapo babu zetu walipolala vitu vyote vinakaa hali iyo hiyo tangu mwanzo wa kuumbwa."
Kuja kwa mpinga Kristo ni dalili ya mwisho wa dunia. imeandikwa, 1Yohana 2:18 "Watoto ni wakati wa mwisho na kama vilelivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja hata sasa wapinga Kristo wengi wamekwisha kuwapo kwa sababu hiyo twajua ni wakati wa mwisho."
Je! Yesu alisema jinsi mwisho utakavyo kuja?. Imeandikwa, Mathayo 24:14, "Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote kuwa ushuhuda kwa mataifa yote hapo ndipo ule mwisho utakapo kuja."
Watu watakuja kwa mfano wa yesu nao watapoteza wengi. Imeandikwa, Mathayo 24:23-24 "Wakati huo mtu akiwaambia tazama Kristo yupo hapa au yuko kule msisadiki. kwa maana watatoke makristo wa uongo nao watatoa ishara kubwa na maajabu wapate kuwapoteza kama yakini hata walio wateule."
Kutakuwa na ishra kaqtika mwezi jua na hata nyota. Imeandikwa, Mathayo 24:29-30 "Lakini mara baada ya dhiki ya siku zile jua litatiwa giza na mwezi hautatoa mwanga wake na nyota zitaanguka mbinguni na nguvu za mbingu zitatikisika. Ndipo itakapoonekana ishara ya mwan wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa ya ulimwengu watakapoomboleza na watamwona mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi."
Je! siku za mwisho zitakua vipi?. Imeandikwa, 2Timotheo 3:1-5 "Lakini ufahamu neno hili ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe wenye kupenda fedha wenye kujisifu wenye kiburi wenye kutukana wasiotii wazazi wao wasio na shukrani, wasio safi wasio wapenda wakwao wasio takakufanya suluhu wasingiziaji wasiojizuia wakali wasio penda mema, wasaliti wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu wenye mfano wa utaua lakini wakikana nguvu zake hao nao ujiepushe nao."
Elimu itaongezeka na watu watasafiri huku na kule. hi ni ishara ya siku za mwisho. Imeandikwa, Danieli 12:4 "Lakini wewe Ee Danieli yafunge maneno haya ukatie mhuri kitabu hata wakati wa mwisho wengi wataenda mbio huku na huko na maarifa ya taongezeka."
Je! Bibilia yaonyesha ishara gani za siku za mwisho? Imeandikwa, Luka 21:25-26 "Tena kutakua na ishara katika jua na mwezi na nyota na katika nchi dhiki ya mataifa wakishangaa kwa uvumi wa bahari na msukosuko wake watu wakivunjika mioyo kwa hofu na kutazaia mambo yatakayoupata ulimwengu kwa kuwa nguvu za mbinguni zitatikisika."
Watu wataongea kuhusu amani hi ni ishara ya siku za mwisho. Imeandikwa, 1Wathesalonike 5:2-3 "Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile wivi ajavyo usiku wakati wasemapo kuna amani na usalama ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba wala hakika hawataokolewa."
Je watu wafanyaje wakati mambo haya yanapo endelea? Imeandikwa, Mathayo 24:42-44 "Kesheni basi kwa maana hajui nisiku gani atakayokuja Bwana wenu lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angalijua ile zamu mwivi atakayokuja angalikesha asingeliasha nyumba yake kuvunjwa. Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari kwa kuwa katika saa msiyo dhani mwana wa Adamu yuaja."
Kuja kwa mpinga Kristo ni dalili ya mwisho wa dunia. imeandikwa, 1Yohana 2:18 "Watoto ni wakati wa mwisho na kama vilelivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja hata sasa wapinga Kristo wengi wamekwisha kuwapo kwa sababu hiyo twajua ni wakati wa mwisho."
Je! Yesu alisema jinsi mwisho utakavyo kuja?. Imeandikwa, Mathayo 24:14, "Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote kuwa ushuhuda kwa mataifa yote hapo ndipo ule mwisho utakapo kuja."
Watu watakuja kwa mfano wa yesu nao watapoteza wengi. Imeandikwa, Mathayo 24:23-24 "Wakati huo mtu akiwaambia tazama Kristo yupo hapa au yuko kule msisadiki. kwa maana watatoke makristo wa uongo nao watatoa ishara kubwa na maajabu wapate kuwapoteza kama yakini hata walio wateule."
Kutakuwa na ishra kaqtika mwezi jua na hata nyota. Imeandikwa, Mathayo 24:29-30 "Lakini mara baada ya dhiki ya siku zile jua litatiwa giza na mwezi hautatoa mwanga wake na nyota zitaanguka mbinguni na nguvu za mbingu zitatikisika. Ndipo itakapoonekana ishara ya mwan wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa ya ulimwengu watakapoomboleza na watamwona mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi."
Je! siku za mwisho zitakua vipi?. Imeandikwa, 2Timotheo 3:1-5 "Lakini ufahamu neno hili ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe wenye kupenda fedha wenye kujisifu wenye kiburi wenye kutukana wasiotii wazazi wao wasio na shukrani, wasio safi wasio wapenda wakwao wasio takakufanya suluhu wasingiziaji wasiojizuia wakali wasio penda mema, wasaliti wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu wenye mfano wa utaua lakini wakikana nguvu zake hao nao ujiepushe nao."
Elimu itaongezeka na watu watasafiri huku na kule. hi ni ishara ya siku za mwisho. Imeandikwa, Danieli 12:4 "Lakini wewe Ee Danieli yafunge maneno haya ukatie mhuri kitabu hata wakati wa mwisho wengi wataenda mbio huku na huko na maarifa ya taongezeka."
Je! Bibilia yaonyesha ishara gani za siku za mwisho? Imeandikwa, Luka 21:25-26 "Tena kutakua na ishara katika jua na mwezi na nyota na katika nchi dhiki ya mataifa wakishangaa kwa uvumi wa bahari na msukosuko wake watu wakivunjika mioyo kwa hofu na kutazaia mambo yatakayoupata ulimwengu kwa kuwa nguvu za mbinguni zitatikisika."
Watu wataongea kuhusu amani hi ni ishara ya siku za mwisho. Imeandikwa, 1Wathesalonike 5:2-3 "Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile wivi ajavyo usiku wakati wasemapo kuna amani na usalama ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba wala hakika hawataokolewa."
Je watu wafanyaje wakati mambo haya yanapo endelea? Imeandikwa, Mathayo 24:42-44 "Kesheni basi kwa maana hajui nisiku gani atakayokuja Bwana wenu lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angalijua ile zamu mwivi atakayokuja angalikesha asingeliasha nyumba yake kuvunjwa. Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari kwa kuwa katika saa msiyo dhani mwana wa Adamu yuaja."
Subscribe to:
Posts (Atom)
